AMUA KUSIMAMIA AFYA YAKO MUDA WOTE.




Habari rafiki,
Karibu kwa mara nyingine kwenye mtandao wa Afya ni yangu,
Kama ilivyozoeleka siku zote sisi kama wanafamilia tunashirikishana yale yaliyomuhimu sana katika sehemu ya maisha yetu ambapo bila sehemu hii ya hatuwezi kuyafurahia maisha kamwe. Sehemu yenyewe si nyingine bali ni AFYA. 

Rafiki chukua hatua mapema ya kusimamia afya yako kuanzia sasa yaani kama umefanikiwa kusoma makala hii yakupasa uanze kutafakari kwa kina kuhusu afya yako sasa, kwa maana ya kwamba hakuna mtu ambaye atakaye kusimamia katika hili ispokuwa wewe binafsi.

Kama tunavyoelewa kuwa asilimia kubwa ya maradhi yanayowakabili watu wengi yanatokana na wao, kwa mfano unapoenda hospitali ukiwa unahisi unadalili zote za malaria na ikathibitishwa na mtu wa maabara kuwa unamalaria jua ya kwamba maralia hiyo haijaingia mwilini siku hiyo yaani haujang’atwa na mbu siku hiyo hiyo na kuuguugua malaria siku hiyo.Kwa maana ya kwamba kuna kitu ulikosea hapo nyuma kuhakikisha unaepuka kuwa na maradhi ya maralia aidha ulikua hutumii chandarua wakati wa kulala, nyumba yako imezungukwa na nyasi ndefu zinazochangia mazalia ya mbu au mazingila unayoishi yamezungungwa na vidimbwi vya maji yaliyotuama ambapo mazalia ya mbu huongeza kwa wingi.


Rafiki afya ni kitu muhimu sana katika maisha yako, bila afya hakuna maisha. Kuna msemo mmoja wa Kiswahili unaosema “thamani ya afya aijuae mgonjwa”. Lakini sisi wanafamilia wa mtandao wa Afya ni yangu tunasema thamani ya afya aijuae ni mimi na wewe.


Kila inapoitwa leo, kila inapoingia asubuhi au kabla ya kuianza siku yako chukua dakika kadhaa kutafakari kuhusu afya yako ndio uanze kufanya shughuri nyingine za kiuchumi, kijamii, kisiasi na kitamaduni. Na kila unachopanga kufanya hakikisha hakiathiri afya yako.


Unatakiwa uishi kama mtu anaemiliki gari, yaani huwezi kuanza kuwasha gari kama hujalikagua gari lako kama lina mafuta ya kutosha, rejecter kama inamaji ya kutosha, mataili kama yanaupepo wa kutosha na hata kuhakikisha kama bima zote pamoja na leseni zipo sawa sawa. Baada ya hapo ndipo utakuwa salama na huru utakapokuwa barabarani.
Hivyo ndivyo ilivyo hata kwenye upande wa afya yako, kuwa makini muda wate kuhakikisha afya yako iko vyema.


 Tunakutakia kila la kheri.


Kwa maoni, ushauri, TIBA na DAWA wasiliana nasi kupitia simu namba 0654502550, 0652028582 au 0654394698.

Whatsap group: AFYA NI YANGU,
Facebook Page: Afya Ni Yangu.

 TRIPLE MINDED.

Jaza form hii kupokea makala za Afya Ni Yangu.

* indicates required
Email Format

No comments:

Post a Comment