MFULULIZO WA MAKALA; VIPINDI VYA MAKALA VITAKAVYORUSHWA KILA SIKU YA WIKI KUPITIA MTANDAO WA ‘AFYA NI YANGU’.



1.  SWALI LA LEO
2.  AFYA BORA
3.  AFYA YA UZAZI
4.  AFYA YA MTOTO
5.  ONGEA NA MSHAURI
6.  MASWALI NA MAJIBU
7.  CHANGAMOTO YA SIKU
8.  KLIINIKI YA MAMA NA MTOTO
9.  HUDUMA YA KWANZA (FIRST AID)
10.              MEDICAL & SURGICAL CONDITIONS

SWALI LA LEO;
Ni kipindi kitakacho fanyika siku ya jumatano, swali ambalo litawekwa mezani na wataalamu wa afya (uongozi wa mtandao wa AFYA NI YANGU). Swali ambalo litakuhitaji ufikiri wa kina ili kupata jibu sahihi, majibu yote  yatakayojibiwa na wanachama wa kundi hili yatafanyiwa kazi na uongozi.

AFYA BORA;
Ni makala itakayo rushwa siku ya jumanne, hii ni aina ya makala itakayo kuongezea maarifa kiundani zaidi kuhusu umuhimu wa kuwa na afya bora, namna gani unaweza kuwa na afya bora wakati wote na kuimarisha afya yako kwa ujumla.

AFYA YA UZAZI;
Ni aina ya makala itakayorushwa siku ya jumatatu, hapa utapata kujifunza magonjwa ya aina yote ya uzazi kwa mwanamke na mwanaume  pamoja na tiba/dawa sahihi.

AFYA YA MTOTO;
Ni makala itayorushwa siku ya alhamisi, itakayozungumzia hasa afya pamoja na magojwa ya watoto kuanzia akiwa kijusi (fetus) – kichanga (Neonate/Infancy) – hadi miaka kumi na moja (Children). Ni siku muhimu sana kwani utapata kuyafahamu mengi kuhusu watoto, kwani watoto ni sehemu ya furaha katika maisha ndoa na familia kwa ujumla.

ONGEA NA MSHAURI;
Huu ni wakati wa mwanachama wa mtandao huu kupata fursa ya kuongea na mshauri moja kwa moja kwa kupiga simu, kwa siku ya jumamosi na jumapili kuanzia saa tano asubuhi hadi saa nne usiku.
Ushauri utakaotolewa ni wa magonjwa ya aina yoyote ya binadamu na kupatiwa ushauri na ufumbuzi wa tatizo husika.

N.B. Hairuhusiwi kutuma ujumbe (sms), hivyo ujumbe utakaotumwa hautafanyiwa kazi na uongozi husika.

MASWALI NA MAJIBU;
Hapa mwanachama atapata fursa ya kuuliza maswali husiana na magonjwa ya aina yote ya binadamu, kipindi hiki ni kwa siku ya Ijumaa tu. Hapa mwanachama atapata fursa ya kuwasilisha swali lake kwa njia ya ujumbe wa wa maandishi (whatsap group, inbox) au kwa kupitia e mail yetu (afyaniyangu@gmail.com)..

CHANGAMOTO YA SIKU;
Hapa utapokea makala itakayo elezea suluhisho la miongoni mwa  changamoto  zinazowasumbuwa watu wengi kuhusu afya zao hasa wale wanaotufikia moja kwa moja na wale wanaotupigia simu pia. Makala hii itaandaliwa siku ya ijumaa pekee. Hivyo tutakushirikisha na tutajifunza kwa pamoja.

KLINIKI YA MAMA NA MTOTO;
Hii ni huduma maalamu itakayotolewa kwa mfumo wa makala kuelezea huduma anazopaswa kupewa mama mjamzito kuanzia anapoingia kliniki hadi anapotoka, vile vile huduma anazopewa mtoto pale anapoingia kliniki hadi kutoka.
Hapa utajifunza mambo mbalimbali kama vile;



  • ·         Maana ya kila huduma anayopewa mama mjamzito anapokuwa kliniki.

    ·         Maana ya kila hatua anayoifuata mama mjamzito anapokuwa kliniki.

    ·         Umuhimu wa dawa/chanjo anazopewa mama akiwa kliniki.

    ·         Elimu anayopewa maam akiwa kliniki.

    ·         Vipimo anavyotakiwa kufanyiwa anapokuwa kliniki na mengine mengi.

Huduma hii ya KLINIKI YA MAMA NA MTOTO itatolewa kwa njia ya mtandao wa facebook page na whatsap ‘Afya Ni Yangu’ kila jumapili kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa nane mchana.

Itafanyikaje kupitia mtandao?

Hapa tutakuwa kliniki na mama, mwanamke na hata wananaume wenye kujali na kuthamini afya za wake zao au wanawake pamoja na mtoto wao mtarajiwa, ili kupata somo hili inakubidi mwanachama awe anatumia kifaa chochote kinachomuwezesha kuwa na mtandao wa kijamii kama vile smartphone au tablet ambapo anatakiwa kuwa online siku hiyo na wakati wa somo husika.

 Itakuwaje kama sipo online kwa muda huo?

Bado hujapoteza kitu moja kwa moja kwani endapo utafungua mtandao wako utakutana na somo lililokuwa likiendelea siku hiyo, ispokuwa utakosa fursa ya kuuliza swali kuhusiana na somo au kile kinachohusiana na Kliniki ya mama na mtoto badala yake sasa utaweza kuuliza swali hilo kwenye kipindi kijacho.

Je, huduma hiyo ni kwa ajili ya wanawake wajawazito na wenye watoto wadogo pekee?

Hapana, huduma hii ni muhimu sana kwa kila mtu yaani mwanaume na mwanamke kwani ni vyema kwa wakina baba kuelewa ni huduma gani ambazo wenzi wao hupewa pindi wanapokuwa kwenye chumba cha uchunguzi na huduma zote wanazopata wanapokuwa kliniki kwa ujumla.

HUDUMA YA KWANZA (FIRST AID)

Hiki ni kipindi ambacho utaweza kujifunza ni kwa namna gani unaweza kutoa huduma ya kwanza kwa mtu yoyote pale tu anapopatwa na tatizo la ghafla la kiafya linalohitaji huduma ya kwanza kabla ya kumfikisha kituo cha afya.
Hili somo ni muhimu sana kwani utakuwa unauwezo wa kuokoa maisha ya mtu endapo tatizo litatokea ghafla eneo lolote ulilopo kama vile nyumbani, shuleni, ofisini, mgahawani, shambani n.k
Maarifa haya utayapata siku ya jumamosi jioni, hivyo utapaswa kuwa makini na somo hili.

MEDICAL & SURGICAL CONDITIONS

Hapa sasa ni ule wakati wakujifunza magonjwa ya kitabibu (kisukari, nimonia, kifua kikuu, mafua, UTI, malaria n.k) na magonjwa ya upasuaji (Kidole tumbo, kuziba kwa utumbo wa chakula, uvimbe n.k
Utapokea maarifa kwa undani zaidi kuhusu magonjwa haya, ambapo itakusaidia kugundua ugonjwa husika, dalili, vipimo vinavyohusika kugundua ugonjwa, tiba yake, namna ya kuepukana na ugonjwa husika.

MUHIMU:

Huu ni utaratibu mpya kabisa wa mfululizo wa masomo ya afya, kwa hakika tutakushirikisha maarifa hayo muhimu sana katika maisha yako ya kila siku na baada ya muda utakuwa na uelewa mpana kuhusu afya na hautakuwa hapo ulipo sasa kifikra. Huu mfumo mpya wa makala za afya umeandaliwa baada ya kufanyia kazi changamoto nyingi tulizokuwa tukipokea, hivyo tunaimani kuwa changamoto ni nyingi ila tutahakikisha tunazifanyia kazi kadri ya uwezo wetu.

Shabaha yetu kubwa ni kuhakikisha unakuwa na AFYA BORA YENYE UHAKIKA siku zote na wakati wote.

TRIPLE MINDED.




Jaza form hii kupokea makala za Afya Ni Yangu.

* indicates required
Email Format

FORM YA KUJIUNGA


Jaza form hii kupokea makala za Afya Ni Yangu.

* indicates required
Email Format

KUPOKEA MAKALA ZA AFYA NI YANGU KUPITIA EMAIL YAKO.

 Habari rafiki,
Kuna baadhi ya email tulizopokea zimeandikwa kimakosa hivyo basi kama hadi sasa hujapokea makala yoyote kutoka mtandao wa Afya Ni Yangu
Bonyeza link hii kujiunga na matandao wa Afya Ni Yako 

Utaona sehemu imeandikwa 'Jazwa form hii kupokea makala za mtandao wa Afya Ni Yangu'. Weka taarifa zako.