AFYA YA MTOTO (1); Homa kwa watoto


 

Habari rafiki,

Tunakubaliana kwa pamoja kuwa watoto ni sehemu ya furaha katika maisha ya ndoa, na hilo tunalisadiki kwa pamoja.

Linapokuja suala la maradhi hasa kwa watoto katika familia hupoteza furaha yote katika familia.

Leo tutakushirikisha kuhusu homa hasa kwa watoto. Homa sio ugonjwa, homa ni dalili ya ugonjwa.

Kumekuwa na baadhi ya wazazi wakiona watoto wao joto la mwili limepanda hutumia dawa za kushusha joto kama vile paracetamol (Panadol), si hatua mbaya ya kuchukua ispokuwa tatizo ni pale joto la mwili linapopanda mara kwa mara kwa zaidi ya siku tatu mfululizo bila kuchukua hatua ya kumpeleka mtoto kituo chochote cha afya kilichopo karibu.

Tuangalie nini maana ya jotomwili (body temperature).

Jotomwili  ni kipimo cha uwezo wa mwili kutengeneza joto, ambapo mwili hutengeneza joto kulingana na msawazo unaotakikana hata kama joto la nje ya mwili yaani mazingira yanayotuzunguka yatabadilika.

Inakuaje ya mwili unachemka?

Joto la mwili linapopanda kuliko kawaida ni kwamba mishipa ya damu (blood vessels) katika ngozi hutanuka na kubeba joto jingi kwenye ngozi ya mwili na kuanza kutokwa jasho kupita kiasi. Na tunaposema homa tunamaanisha kupanda kwa jotomwili (fever).

Ipi njia sahihi ya kutambua jotomwili limepanda?

Kuna njia ya asili ambayo tumeshaizoea kuitumia kugundua jotomwili limepanda au la, kwa kutumia sehemu ya juu ya kijanja cha mkono (dorsum) na kugusicha kwenye mwili wa mgonjwa. Ni njia nzuri ya awali katika kugundua jotomwili ispokuwa inakuwa ngumu kugundua joto la mwili limepanda kwa kiasi gani.

Njia iliyo ya uhakika ni kutumia kifaa kinachoitwa kipima joto (clinical thermometer), hiki ni kifaa kinachotumiwa hasa na wataalamu wa afya kwenye vituo vya afya. Kifaa hiki ni muhimu kwa kila familia kuwa nacho kwani ni rahisi kukitumia na kukielewa.

Utajuaje jotomwili limepanda kwa kutumia kifaa hicho (clinical thermometer)?

Kuna aina kama mbili za kipimajoto, ya kwanza ni mercury thermometer nay a pili ni digital thermometer. Kwa matumizi ya nyumbani ni vyema kutumia digital thermometer kwa urahisi wa kupata matokeo ya jotomwili.

Kiwango cha jotomwili.

Jotomwili la kwaida ni nyuzi joto 36.5 hadi 37.5, ikitokea kipima joto kikaonesha ni zaidi ya nyuzi joto 37.5 ni dalili ya kupanda kwa jotomwili, hivyo yakupasa kumpeleka mtoto kwenye kituo chochote cha afya kilichopo karibu.

Muhimu; 

Kupanda kwa jotomwili kwa watoto ni dalili ya hatari ukilinganisha na watu wazima, endapo hatua stahiki hazitachukuliwa hupelekea mtoto kupata degedege (convulsion), hivyo basi yakupasa kumpeleka kwenye kituo chochote cha afya kilichopo karibu yako.

Tukutane tena kwenye kipindi kijacho cha makala zinazohusu AFYA YA MTOTO siku kama ya leo, vilevile tutakutana kesho kwenye kipindi cha makala zinazoendelea.

Tunakutakia kila la kheri

Kwa maoni, ushauri, TIBA NA DAWA, Piga simu namba: 0652028582 au 0652394698 au 0654502550.

Whatsap group: Afya Ni Yangu,


Facebook Page: Afya Ni Yangu.


#TRIPLE MINDED.


 

Jaza form hii kupokea makala za Afya Ni Yangu.

* indicates required
Email Format

No comments:

Post a Comment