AFYA YA UZAZI (1); Kuwahi kufika kileleni wakati wa tendo la ndoa kwa wanaume (Premature ejaculation).


Habari rafiki,
Ni matumaini yetu kuwa umeinza siku yako vyema kabisa ukiwa na afya njema, tuna kila sababu ya kukupongeza kwa hilo kwani si kila aliyeianza siku ya leo anaafya njema kwani afya njema inatengenezwa na haiji kwa bahati.

Leo ni ile siku yetu maalumu ya kupeana maarifa kuhusu afya ya uzazi kama ilivyodesturi yetu. Katika somo letu la leo tutajifunza kuhusu tatizo la kuwahi kutoa mbegu za uzazi (manii) au kufika kileleni kwa wanaume punde tu mwanaume anaponza kushiriki tendo la ndoa.

Kama tunavyofahamu kuwa hili ni tatizo na limekuwa likiathiri idadi kubwa ya wanaume kwa sasa na limekuwa na tafsiri tofauti katika jamii yetu na hata kupelekea baadhi ya ndoa kuvunjika.

Tuungane kwa pamoja tukajifunze somo hili……

Kuwahi kutoa manii mapema baada tu ya kunza tendo la ndoa kwa kitaalamu tunaita (Premature ejaculation) ni kitendo cha kutojizuia kutoa manii aidha kabla au baada ya sekunde chache kuanza kwa tendo la ndoa.

Tatizo hili husababisha kutokuridhika au kutofurahia tendo la ndoa kwa wanandoa wote wawili (mwanaume na mwanamke). Na hali hii husababisha uoga kwa wanandoa na kupelekea kuongezeka kwa tatizo maradufu.

Ni sababu gani hasa husababisha kuwahi kufika kileleni (premature ejaculation)?

Mpaka sasa hakuna sababu za moja kwa moja zinazosababisha kuwahi kufika kileleni kwa mwanaume (orgasm).

Wakati mwengine tatizo hili hutokana na hali ya mazingira wakati wa tendo la ndoa, uoga uliopitiliza (anxiety), msongo wa mawazo (depression).

Vile vile husababishwa na tatizo la vichochezi vya mwili vinavyohusika na uzazi (hormonal problems), majeraha hasa sehemu za kichwa (brain injury) na hata matokeo yasiyotarajiwa kwa baadhi ya dawa (drug side effects).

Ni zipi dalili za kuwahi kufika kileleni (orgasm) kwa wanaume?

Dalili kubwa ni kushindwa kujizuia kutoa manii kabla au muda mfupi baada ya kuanza tendo la ndoa, kutoka kwa manii pasipo mwanaume kutarajia.

Tiba yake ni ipi?

Kwa baadhi ya wanaume tatizo hili hupotea baada ya muda mrefu, kwa wanaume wanaotumia kilevi aina ya pombe au kuvuta sigara wanatakiwa kuacha mara moja na inaweza kuimarisha utoaji manii mzuri.

Vile vile zipo dawa za kuondoa tatizo hilo mara moja na kuimarisha mfumo mzuri wa mwanaume wa utoaji manii wakati wa tendo la ndoa na kupelekea kumridhisha mwenza wake na kufurahia tendo la ndoa.

Hapo tumefikia mwisho rafiki katika somo letu siku ya leo, tukutane tena kwenye mwendelezo wa masoma ya afya ya uzazi wiki ijayo siku kama ya leo. Pia tutakutana tena kesho kwenye kipindi cha makala ya AFYA BORA.

Tunakutakia kila la kheri,

“Afya bora ndio msingi wa mafanikio yako”

Kwa maoni, ushauri, TIBA NA DAWA, Piga simu namba: 0652028582 au 0652394698 au 0654502550.
Whatsap group: AFYA NI YANGU,
Facebook Page: Afya Ni Yangu.

#TRIPLE MINDED.

 Jaza form hii kupokea makala za Afya Ni Yangu.

* indicates required
Email Format

No comments:

Post a Comment