Habari rafiki,
Karibu kwa mara nyingine kwenye mtandao wa Afya ni yangu,
Kama ilivyozoeleka siku zote sisi kama wanafamilia
tunashirikishana yale yaliyomuhimu sana katika sehemu ya maisha yetu ambapo
bila sehemu hii ya hatuwezi kuyafurahia maisha kamwe. Sehemu yenyewe si
nyingine bali ni AFYA.
Rafiki chukua hatua mapema ya kusimamia afya yako kuanzia sasa
yaani kama umefanikiwa kusoma makala hii yakupasa uanze kutafakari kwa kina
kuhusu afya yako sasa, kwa maana ya kwamba hakuna mtu ambaye atakaye kusimamia
katika hili ispokuwa wewe binafsi.
Kama tunavyoelewa kuwa asilimia kubwa ya maradhi
yanayowakabili watu wengi yanatokana na wao, kwa mfano unapoenda hospitali
ukiwa unahisi unadalili zote za malaria na ikathibitishwa na mtu wa maabara
kuwa unamalaria jua ya kwamba maralia hiyo haijaingia mwilini siku hiyo yaani
haujang’atwa na mbu siku hiyo hiyo na kuuguugua malaria siku hiyo.Kwa maana ya
kwamba kuna kitu ulikosea hapo nyuma kuhakikisha unaepuka kuwa na maradhi ya
maralia aidha ulikua hutumii chandarua wakati wa kulala, nyumba yako
imezungukwa na nyasi ndefu zinazochangia mazalia ya mbu au mazingila unayoishi
yamezungungwa na vidimbwi vya maji yaliyotuama ambapo mazalia ya mbu huongeza
kwa wingi.
Rafiki afya ni kitu muhimu sana katika maisha yako, bila afya
hakuna maisha. Kuna msemo mmoja wa Kiswahili unaosema “thamani ya afya aijuae
mgonjwa”. Lakini sisi wanafamilia wa mtandao wa Afya ni yangu tunasema thamani
ya afya aijuae ni mimi na wewe.
Kila inapoitwa leo, kila inapoingia asubuhi au kabla ya
kuianza siku yako chukua dakika kadhaa kutafakari kuhusu afya yako ndio uanze
kufanya shughuri nyingine za kiuchumi, kijamii, kisiasi na kitamaduni. Na kila
unachopanga kufanya hakikisha hakiathiri afya yako.
Unatakiwa uishi kama mtu anaemiliki gari, yaani huwezi kuanza
kuwasha gari kama hujalikagua gari lako kama lina mafuta ya kutosha, rejecter kama
inamaji ya kutosha, mataili kama yanaupepo wa kutosha na hata kuhakikisha kama bima
zote pamoja na leseni zipo sawa sawa. Baada ya hapo ndipo utakuwa salama na
huru utakapokuwa barabarani.
Hivyo ndivyo ilivyo hata kwenye upande wa afya yako, kuwa
makini muda wate kuhakikisha afya yako iko vyema.
Tunakutakia kila la
kheri.
Kwa maoni, ushauri, TIBA na DAWA wasiliana nasi kupitia simu
namba 0654502550, 0652028582 au 0654394698.
Whatsap
group: AFYA NI YANGU,
Email: afyaniyangu@gmail.com
Facebook Page: Afya Ni Yangu.
TRIPLE MINDED.